www.shijamovies.blogspot.com

www.shijamovies.blogspot.com

Marine Tanzania Swimming Club Call: +255 655 461 460

Marine Tanzania Swimming Club Call: +255 655 461 460
Get Swimming Training from Experts www.marineswimmingclub.blogspot.com

January 28, 2014

TWANGA PEPETA YAPATA PIGO

kundi la muziki wa dansi hapa nchini African Stars "Twanga Pepeta" limepata pigo baada ya msanii mwenzao  Soud Mohammed Said “MCD” kufarilki dunia Mkoani Kilimanjaro. MCD alikuwa ni msanii mahiri wa kupiga drum. Mungu ailaze roho ya marehemu MCD mahala pema peponi Amen!

MAYUNGA KUJA NA SUGAR CANE

 Msanii chipukizi katika kiwanda cha filamu bongo ambaye anatoka Mkoani Geita Suleiman Mayunga anakaribia kuachia filamu yake inayokwenda kwa jina la sugar cane.

 Suleiman Mayunga Negena katika filamu yake  ya kwanza.



Mayunga ambaye alifanya vizuri sana katika filamu ya mistake vision amesema nia ya kufanya vizuri ni kutaka kuwaonyesha watanzania na waandaaji wa filamu za bongo kuwa Mkoani Geita kuna vipaji kibao.




January 24, 2014

Kitale atoa kibao kipya Kitale Feat Mide-(nawaektia)

 PICHA KIBAO ZA BEHIND THE SIN YA VIDEO YA NGOMA MPYA YA KITALE Feat MIDE-(Nawaektia) COMING SOON...


Jela kwetu c disco


Uvutaji wa ganja sina mpango nao!!!





January 23, 2014

AFYA YA JOHARI NI TETE

Mwana Dada na mwigizaji mkongwe Blandina Chagula maarufu Johari ni mgonjwa na amelazwa katika moja ya hospitali maarufu hapa jijini. 


 Ndugu wa karibu wa Johari ameshindwa kuweka wazi ni hospitali gani ambayo Johari amelazwa na kusema kuwa wanashindwa kusema mahali alipolazwa Johari kutokana na usumbufu wa waandishi wa habari " kwakweli Johari anaumwa sana na tunaomba dua zenu tu" Alisema ndugu huyo wa johari.


January 22, 2014

WEMA KAMA ZAMANI.

Mrembo na mwigizaji wa filamu za bongo Wema Isaac Sepetu amefunguka na kusema kuwa pamoja na kunyang'anywa vitu na mpenzi wake wa zamani amesema kuwa hana shida tena kwani mpenzi wake diamond anakwenda kununua kila kitu kilichochukuliwa.


siku za hivi karibuni Wema amejikuta kwenye mkasa huo baada ya kutangaza kurudiana na mpenzi wake wa zamani diamond.




January 20, 2014

HANS WA LEO KIBOKO.

Msanii chipukizi katika gemu la muziki wa kizazi kipya Hans ameanza vizuri kwa kuachia ngoma yake mpya inayojulikana kwa jina la THAMANI.


Katika wimbo huo Hans amemshirikisha msanii kutoka katika kundi la THT Amini. 


Kwa sasa ngoma hiyo inapigwa kila kona ya mtaa.




NASRI SPIDI MIA.

Msanii wa muziki wa kizazi kipya NASRI TAJIRI ni msanii anayekuja kwa kasi ya ajabu na kuwafanya wasanii wakongwe wa muziki wa bongo fleva kumuogopa.

Nasri ambaye  siku hizi za karibuni amekula mkataba wa TSH 15,000,000 na moja ya makampuni makubwa hapa nchini  kwa  sasa anatamba na kibao chake kinachojulikana kama NYAMIHELA.


Ngoma hiyo ya NYAMIHELA kwasasa inapigwa kila REDIO na TV.




January 17, 2014

SHIJA KUACHIA LAZY BOY.

Baada ya kukaa kimya kwa muda mrefu Mwigizaji wa filamu hapa nchini Deogratius Shija anatarajia kuachia filamu yake mpya inayokwenda kwa jina la LAZY BOY


Katika filamu hiyo Shija amewashirikisha wasanii mahiri kama vile Jackline Wolper “gamble" Saimon Mwapagata” Rado" na Joseph mteme "Baga" Shija anasema kuwa kimya chake kilikuwa kina mshindo mkubwa sana kwani lazy boy ni moja ya filamu Kali sana.


Shija amewataka mashabiki wake wakae tayari kuipokea  Lazy boy itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.


January 15, 2014

KALI YA MONALISA.

Mwigizaji wa siku nyingi na nyota wa kundi la zamani la Nyota Ensemble "mambo hayo" Yvone cherry” Monalisa" amewashauri wasanii wenzake kutoanika mambo yao hadharani . Monalisa amesema kuwa si busara kwa msanii ukaweka mambo yako hadharani na kufahamika na watu.


monalisa ni msanii pekee hapa nchini asiyekuwa na kashfa kwenye magazeti pendwa.kwasasa mwanadada huyu anatamba katika tamthilia ya siri ya mtungi.

January 14, 2014

VIDEO YA TUPOGO BADO SANA.

Msanii wa mziki wa bongo fleva Omary Nyembo "Ommy Dimpoz" amesema video ya wimbo wake wa tupogo bado hajaiandaa mpaka baadae kidogo. 
 Ommy dimpoz anatarajia kuachia audio ya nyimbo wake mpya muda wowote.wimbo wa tupogo ni moja ya nyimbo Kali zinazopigwa katika redio mbali mbali hapa nchini.


January 13, 2014

SNURA AWAPA RAHA WATOTO YATIMA

Msanii wa filamu na mwimbaji wa mziki wa bongo fleva Snura Mushi Jana katika kusheherekea Siku yake ya kuzaliwa aliamua kwenda kwenye kituo cha kulelea watoto yatima na kula nao bata.

 Snura ambaye ameisha cheza filamu kibao kwa sasa Mwana Dada huyu mwenye kiuno cha ajabu anapokuwa jukwaani anatamba na kibao chake kijulikanacho kama nimevugwa. Happy birthday Snura
.



January 10, 2014

MPOTO AWAITA

Msanii maarufu wa nyimbo za mashairi nchini Mrisho Mpoto ameachia kibao chake kipya kijulikanacho kama WAITE ambacho kwa sasa kinapigwa katika redio zote hapa nchini.


Mrisho Mpoto ni msanii ambaye amejipatia umaarufu mkubwa katika nyimbo yake ya salamu zangu Mjomba. Kwasasa Mrisho anamiliki bendi ya Mjomba band. 



Siku za hivi karibuni mrisho alitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la songea kwa tiketi ya Chadema.



January 9, 2014

PROFESA JAY ATANGAZA NIA YA KUGOMBEA UBUNGE.

Msanii nguli wa muziki wa bongo freva Joseph Haule "Prof Jay” ametangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la kinondoni kupitia chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA 2015.


Huu ni mwendelezo wa wasanii wa bongo freva kutangaza nia ya kugombea ubunge kwani siku za hivi karibuni Seleman Msindi "Afande Sele" alitangaza nia ya kugombea ubunge jimbo la Morogoro kwa tiketi ya CHADEMA




January 7, 2014

MZEE KAMBI AKERWA NA MASTAR WAKIKE.

Mwagizaji wa filamu hapa nchini Mzee Hashim Kambi anasikitishwa na kitendo cha wasanii wa kike hapa nchini kuwa ni watu wasumbufu sana wanapokuwa location. Mzee Kambi ameendelea kufunguka bila kumtaja jina la star yoyote ila amesema karibu wasanii wote wa kike ni wasumbufu " msanii anaweza wakati mwingine akakuzimia simu na asije kabisa kufanya kazi na wakati mwingine akaja amechelewa na akifika hana Mudi ya kufanya kazi" Mzee Kambi amesema matatizo haya ya wasanii wa kike hufanya garama za production kuongezeka mara mbili. Mzee Kambi ameshauri wasanii ufike wakati wakajitambua wao wakina nani?

January 6, 2014

STEVEN NYERERE AWAPA RAHA BONGO MOVIE

Mwenye kiti mpya wa bongo movie club bwana Steven Nyerere amewapa raha wasanii wenzake baada ya kuandaa tafrija Kali baada ya kuteuliwa kuwa m/kiti mpya wa bongo movie.

  Baada ya kutangazwa kuwa mshindi Steve Nyerere aliwaambia wanachana wote wa bongo movie hakuna kuondoka na kuwanunulia vinywaji pamoja na muziki kutoka kwenye bendi ya mwanamuziki TID.





January 4, 2014

CHUCHU HANS AWASHANGAZA BONGO MOVIE

Msanii wa filamu hapa nchini leo ameshangaza wasanii wenzake wa filamu baada ya kuingia viwanja vya leaders akiwa na gari la VINCET KIGOSI aina ya land cruiser VX wengi hawakuamini kumuona Chuchu Hans akiwa kwenye gari la Ray.


Siku za hivi karibuni ray na CHUCHU HANS inasemekana wamekuwa kwenye mahusiano ya kimapenzi na kusababisha penzi la Ray na Mainda kuvunjika.


BONGO MOVIE YAPATA UONGOZI MPYA.

Bongo movie yapata uongozi mpya club ya bongo movie hapa nchini imepata uongozi mpya baada ya kufanya uchaguzu wao katika viwanja vya Leaders jijini Dar. Mwenyekiti STEVEN NYERERE


Makamu mwenyekiti MAUNSEIN AWADHI "Dr cheni" 


Katibu mkuu WILIAM MTITU 



 Katibu msaidizi DEVOTHA MBAGA 


Mtunza hazina ISSA MUSA “cloud" 

 

 Msaidizi wake ni CATHY RUPIA



January 2, 2014

UCHAGUZI WA BONGO MOVIE WAANZA KWA MBWEMBWE

Uchaguzi wa viongozi katika club ya bongo movie unit umeanza kwa mbwembe baada ya viongozi wanaotarajia kugombea nafasi mbali mbali kupewa nafasi ya kumwaga Sera mbele ya wapiga kura wao leo katika viwanja vya Leaders club.


Nafasi zinazogombewa ni M/kiti ,Makamu m/kiti katibu,katibu msaidizi na mweka hazina nafasi hizo zilikuwa zimeshikwa na m/kiti ni VINCET KIGOSI "ray"makamu m/kiti IRENE UWOYA katibu alikuwa ni CHIKI MCHOMA na mweka hazina alikuwa SINGLE MTAMBALIKE "Richie Richie".

Watu wanaopewa nafasi ya kushinda ni DR CHENI anayegombea nafasi ya M/kiti wa Club na ISSA MUSA anagombea nafasi ya katibu wakati WILLAM MTITU naye anagombea nafasi ya M/kiti wa club uchaguzi huo unatarajia kufanyika Jumapili hii ya tarehe 5 January 2014.