www.shijamovies.blogspot.com

www.shijamovies.blogspot.com

Marine Tanzania Swimming Club Call: +255 655 461 460

Marine Tanzania Swimming Club Call: +255 655 461 460
Get Swimming Training from Experts www.marineswimmingclub.blogspot.com

May 7, 2014

LINAH:NAFUNGA NDOA MDA SI MREFU

MSANII mwenye sauti mwanana anayetesa kwenye Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’, amefunguka kuwa, ndoa yake na mpenzi wake Nagari Kombo ‘Kaka wa Bongo’ inanukia.


 Msanii mwenye sauti mwanana anayetesa kwenye Bongo Fleva, Estelina Sanga ‘Linah’.
“Sina haja ya kuendelea kumficha mpenzi wangu, kwani kwa sasa anatambulika kwa kila mtu na hasa ndugu zangu wa karibu, kitu cha kusubiriwa kwa sasa ni tarehe ya ndoa yetu tu,” alisema Linah.


Linah akipozi na mpenzi wake Nagari Kombo wakati wa utoaji tuzo za Kili.
Linah alisema hayo wikiendi iliyopita aliponaswa akijiachia na Kaka wa Bongo katika Ukumbi wa Mlimani City, Dar ambapo mpango mzima wa Tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards 2013 – 2014 ulikuwa ukifanyika.


Lina akiwa na mpenzi wake.
Kaka wa Bongo alijizolea umaarufu siku za nyuma baada ya kuingia uwanjani na kumkumbatia mchezaji, Ricardo Kaka wa Timu ya Taifa ya Brazil iliyokuwa ikichuana na Taifa Stars katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.


No comments:

Post a Comment